Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, July 25, 2015

MWINYI KAZIMOTO AREJEA SIMBA



SIMBA ya Dar es Salaam ipo katika harakati za kuimarisha kikosi chake na sasa imefanikiwa kumrejesha nyumbani kiungo wake Mwinyi Kazimoto.
Kazimoto aliyekuwa akichezea klabu ya Al Markhiya ya Qatar, amerejea kwenye klabu hiyo baada ya mkataba wake na klabu hiyo ya Qatar kumalizika.
“Tumemalizana naye kijana, amesaini mkataba wa miaka miwili, naamini mambo yatakuwa sawa. Dhamira yetu ni kuimarisha kikosi chetu,” kilisema chanzo cha kuaminika ndani ya Simba.
Mtoa habari huyo alieleza kuwa wanaamini kusajiliwa kwa Kazimoto kutaifanya Simba kuwa na kikosi imara zaidi, ambacho kitarejesha hadhi ya klabu hiyo.
Hata hivyo Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Haji Manara alipoulizwa jana kuhusiana na habari hizo alisema hafahamu lolote.
“Hapana waone watu wa Kamati ya Usajili ya Simba, mimi sifahamu lolote ndugu yangu,” alisema Manara.
Mapema mwezi huu, Simba ilimrejesha mshambuliaji Mussa Hassan Mgosi akitokea Mtibwa Sugar ya Morogoro. Mgosi kama ilivyokuwa kwa Kazimoto naye aliwahi kuchezea Simba miaka ya nyuma.
Kazimoto aliyejiunga na Simba SC mwaka 2011 akitokea JKT Ruvu, aliuzwa mwaka  2013, Al Markhiya, ambayo ipo Ligi Daraja la Pili nchini humo.
Wachezaji wengine wa hapa nchini waliosajiliwa Simba hadi sasa licha ya Mgosi na Kazimoto ni Peter Mwalyanzi kutoka Mbeya City, Mohamed Fakhi kutoka JKT Ruvu na Samih Haji Nuhu kutoka Azam FC.
Pia Simba imemsajili mshambuliaji wa Vital ‘O ya Burundi, Laudit Mavugo na mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Hamisi Kiiza.

No comments:

Post a Comment