Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, July 30, 2015

MATUIDI NA ZLATAN IBRAHIMOVIC WA PARIS SAINT-GERMAIN WAILIZA UNITED USA NA KUTWAA KOMBE INTERNATIONAL CHAMPIONS CUP

Manchester United wameshindwa kutetea Taji lao la International Champions Cup baada ya kufungwa 2-0 na Paris Saint-Germain kwenye Mechi yao ya mwisho Usiku wa kuamkia Leo huko Soldier Field, Chicago, USA na kuiacha PSG ikibeba Kombe hilo.PSG walifunga Bao lao la kwanza katika Dakika ya 25 baada Mpira mrefu kutoka kwa Silva kumkuta Kipa David De Gea akiwa nafasi ovyo na Blaise Matuidi kuutokea na kufunga.Dakika 9 baada PSG walifunga Bao la Pili kupitia kupitia Straika wao hatari Zlatan Ibrahimovic aliepokea pasi kutoka kwa Lucas Moura na kumpa Maxwell alietumbukiza Krosi ndani ya boksi na kuunganishwa wavuni na Ibrahimovic.
Hadi Mapumziko PSG 2 Man United 0.
Mechi hii ilikuwa ni mechi ya 4 na ya mwisho kwa Man United wakiwa Ziarani huko USA na walishinda mechi zao 3 za awali kwa kuziangusha Club America ya Mexico (1-0), San Jose Earthquakes ya USA (3-1) na Barcelona (3-1).Katika mchezo huo kukaba ndio ilikuwa nguzo!!
Zlatan Ibra
Michael CarrickDepayNdani ya Uwanja wa Soldier Field, Chicago, United States
Manchester United  mpaka sasa hajapata bao, Paris Saint-Germain wanaongoza bao 2-0 zilizofungwa kipindi cha kwanza dakika ya 25 na Blaise Matuidi na lilie la dakika ya 34 na  Zlatan Ibrahimovic.

No comments:

Post a Comment