Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, June 30, 2015

U15 YAREJEA DAR

Kikosi cha timu ya Taifa cha vijana wenye umri chini ya miaka 15 (U-15) leo kinarejea jijini Dar es salaam kikitokea mkoani Mbeya ambapo jana kiliibuk ana ushindi wa ushindi wa mabao 4-1.

U15 ambayo inaandaliwa kwa ajili ya kuwania kufuzu kwa fainali za vijana chini ya miaka 17 barani Afrika kilikua na ziara ya michezo ya kirafiki miwili jijini Mbeya ambapo katika mchezo wa awali pia kiliibuka na ushindi wa mabao 3-0.

Mara baada ya kurejea leo jioni jijini Dar es salaam, kambi ya timu hiyo itavunjwa mpaka watakapokutana tena mwisho wa mwezi ujao kwa ajili ya kuelekea visiwani zanzibar kwa jili ya michezo ya kirafiki.

Lengo la michezo hiyo ya kirafiki ni kutoa nafasi ya kocha Bakari Shime kutambua uwezo wa vijana wake na kuongeza wachezaji wengine katika kikosi hicho kisha kuandaa kikosi bora kitakachoshirki kuwania kufuzu kwa fainali hizo zitakazofanyika nchini Madagascar mwaka 2017.

No comments:

Post a Comment