Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, October 30, 2014

KOMBE LA DUNIA 2018 LITAFANYIKA RUSSIA SEPP BLATTER AANIKA NEMBO YA FAINALI HIZO.

RAIS wa FIFA Sepp Blatter ameiweka hadharani Nembo mahsusi kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2018 ambazo zitachezwa Nchini Russia.
Blatter, akianua rasmi Nembo hiyo kwenye Kipindi maalum cha TV ya Russia huku akisaidiwa na Wanaanga wa Kirusi wanaosafiri kwenda Anga ya juu na mbali kabisa, alisema Nembo hiyo inaonyesha moyo na ari ya Russia.
Baada ya kutamka hivyo, Nembo hiyo ilianikwa hadharani hewani kwenye Matangazo hayo ya TV na Wanaanga hao wa Kirusi ambao walikuwa juu kwenye Anga ya mbali kabisa toka Duniani wakiwa kwenye Chombo chao maalum kiitwacho ‘International Space Station’ ambacho kinazunguka huko juu Angani.
Nembo hiyo inaonyesha Kombe la Dunia likiwa na Rangi Nyekundu na Bluu, Rangi za Bendera ya Russia, likizungukwa na utepe wa Dhahabu.
Russia hawajawahi kuwa Wenyeji wa Kombe la Dunia na pia hawajahi kulitwaa Kombe hili katika Historia yao.
Fainal hizo za huko Nchini Russia Mwaka 2018 zinafuatia zile za kule Brazil zilizochezwa Juni na Julai Mwaka huu na Germany kuibuka Mabingwa wa Dunia.
Fainali nyingine za Kombe la Dunia zitakuwa Mwaka 2022 huko Nchini Qatar.

No comments:

Post a Comment