Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, October 9, 2014

Gareth Bale hataki Cristiano Ronaldo aondoke Real Madrid



Gareth Bale amesema hataki kuona nyota mwenzake Cristiano Ronaldo akiondoka Real Madrid kurudi Uingereza kwenye ligi ya Premier.
Licha ya Ronaldo kuendelea kufunga mabao ikiwemo matatu wikendi jana dhidi ya Athletic Bilbao yaliomfanya afikishe rekodi ya ‘hat-trick’ ya 22 katika La Liga  na kufikia rekodi  ya ligi iliyowekwa na wachezaji wa zamani Telmo Zarra na Alfredo Di Stefan.

Ronaldo amekuwa katika uvumi wa kutaka kurudi katika timu yake ya zamani ya  Manchester United msimu ujao wa kiangazi.
Hivi majuzi, zilizuka tetesi kuwa Ronaldo anaweza kurudi katika timu yake ya zamani ya United ua Manchester City na Bale ametangaza hataki nyota mwenzake arudi kwenye ligi ya Premier.
Amedhihirisha ni mchezaji wa kiwango cha kimataifa amekuwa anafunga mabao mengi.
Bila shaka, hatutaki aondoke na ninataka asalie hapa Real Madrid,” Bale alisema.

No comments:

Post a Comment