Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, October 9, 2014

BECKERNBAUER ASHANGAA QATAR KUPEWA UWENYEJI WA KOMBE LA DUNIA


Franz Beckenbauer amesema alishangazwa na hatua ya Qatar kushinda maandalizi ya kombe la dunia mwaka 2022.
Mchezaji huyo wa zamani wa kikosi cha Ujerumani ni miongoni mwa watu 22 walioamua ni wapi kinyang'anyiro hicho cha mwaka 2018 na 2022 kitafanyika katika kura iliofanyika mnamo mwezi Disemba mwaka 2010.
Akizungumza katika mkutano wa kuimarisha mchezo huo, mwaka 2014 ,Beckenbauer alikataa kusema ni nani aliyempigia kura ,ijapokuwa ilidaiwa kuwa alipendelea  fainali hizo zifanyike nchini Australia.
''Ilikuwa ni kura ya siri,nilishangaa kuona Qatar ikiibuka mshindi'',Alisema mchezaji huyo mkongwe.
Mchezaji huyo wa zamani ambaye alishinda kombe la dunia kama mchezaji na meneja wa timu ya Ujerumani ,aliongezea kuwa,ushindani ulikuwa mzuri,kama ile mingine lakini hakukuwa na tofauti kubwa.
Lazima kuna sababu kwa nini zile nchi nyengine hazikufanikiwa kuandaa fainali.
Beckernbeur enzi za uchezaji wake
Qatar iliishinda Australia,Japan ,korea kusini na Marekani katika kura ya kuandaa fainali za kombe la dunia  mwaka 2022,huku Urusi ikiishinda Uingereza pamoja na Ubelgiji na Uholanzi,Ureno na Uhispania kwa haki ya kuandaa kombe la dunia la mwaka 2018.
Ni kamati kuu ya FIFA ndiyo iliyotoa uamuzi huo ambao umekumbwa na utata tangu tangazo hilo lifanywe.
Wanachama wawili wa zamani wa Shirikisho hilo walizuiliwa kushiriki katika kura hiyo kutokana na madai ya ufisadi,huku wengine sita wakilazimishwa kujiuzulu baada ya kura hiyo.
Backenbauer alijiondoa katika kamati hiyo mnamo mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment