Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, December 14, 2013

MANCHESTER CITY YAIFUNGA ARSENAL 6-3 LEO


Manchester City Wakicheza kwenye uwanja wao wa nyumbani Etihad wamefunga timuya Arsenal bao mbili kipindi cha kwanza cha dakika 45, Bao zilizofungwa na Sergio Agüero dakika ya 14 na Álvaro Negredo dakika ya 39, wao Arsenal wamepata bao lao dakika ya 31 bao la kizembe lililofungwa na Theo Walcott dakika ya 31. Mpaka sasa ni kipindi cha pili City wanaongoza bao 3-1. Bao la tatu likifungwa na Fernandinho kipindi cha pili dakika ya 50 baada ya kuachia shuti kali lililompita mlinda mlango wa Gunners Wojciech Szczesny. Dakika ya 66 David Silva akaifungia bao la nne Manchester City na kufanya bao 4-2 baada ya Theo Walcott kufunga dakika ya 63 bao jingine la pili dakika tatu kupita.Fernandinho akaiongezea tena bao City na kufanya 5-2 dakika ya 88, Bao la tatu kwa Gunners limefungwa na Per Mertesacker dakika ya 90' +4. Dakika za lala salama dakika ya 90 Yaya Touré akaifungia bao la mwisho kwa mkwanju wa penati dakika 90' +6'. Ushindi huu unawapandisha City nafasi ya pili kwenye msimamo wakiwa na alama 32 chini ya Gunners waliopoteza leo wakiwa na alama 35, pointi tatu tu nyuma yao. Nafasi hiiitategemea Liverpool na Chelsea kama watashinda watakaa juu na kama watapoteza City itaendelea kusika nafasi hiyo ya pili.
Majanga kwa Arsenal...
Aguero...yes yes yes!

Dakika ya 14 tu City walikuwa wameisha tupia bao la kwanza

Aguero akishangilia bao lake la dakika ya 14 kwenye uwanja wao wa nyumbani Etihad

Theo Walcott akisawazisha hapa kwa kufanya 1-1 kipindi cha kwanza

Walcottakishangilia baada ya kuisawazishia bao Gunners

Alvaro Negredo akifunga bao la pili nakufanya 2-1 kipindi cha kwanza mwishoni

City wakimwagiana salaam za kupongezana baada ya Negred  kutupia bao la pili
Wachezaji wa Cuty wakipongezana baada ya kufunga bao la nne, bao la David Silva dakika ya 66. Mesut Ozil (kulia) na David Silva (kushoto)wakichuana kipindi cha pili.

Fernandinho akifunga bao la tatu na kufanya 3-1

Fernandinho akiwapa mashabiki mkono baada ya kufunga.

Walcott ndie aliyewapa bao la pili Arsenal 3-2

David Silvaakibusu mkono baada ya kutupia dakika za majeruhi

Fernandinho akifunga bao lake dakika za majeruhi dakika ya 88th na kipa wa Gunners Wojciech Szczesny kutoona ndani yake
Fernandinho baada ya kuiua Gunners dakika za lala salama
VIKOSI:
Manchester City:  Pantilimon, Zabaleta, Kompany, Demichelis, Clichy, Fernandinho, Yaya Toure, Nasri (Garcia 90), Silva (Milner 71), Aguero (Navas 49), Negredo
Subs not used: Hart, Lescott, Kolarov, Dzeko
Booked: Silva, Kompany
Goals: Aguero 14, Negredo 39, Fernandinho 50, 88 Silva 66, Toure 90 (pen)
Arsenal: Szczesny, Sagna, Mertesacker, Koscielny (Vermaelen 42), Monreal, Flamini (Gnabry 72), Wilshere, Ramsey, Ozil, Walcott, Giroud (Bendtner 76)

Booked: Szczesny
Subs not used: Fabianski, Vermaelen, Arteta, Rosicky, Cazorl
Goals: Walcott 31, 63, Mertesacker 90



MSIMAMO WA TIMU TANO ZA JUU KWA SASA BAADA YA MECHI HII YA CITY KUISHA. 
Premier League
Pos.Logo &TeamPWDLGDPts
1ArsenalArsenal1611231635
2Manchester CityManchester City1610242932
3LiverpoolLiverpool159331630
4ChelseaChelsea159331330
5EvertonEverton15771928



RATIBA/MATOKEO
Jumamosi Desemba 14

Man City 6 v Arsenal 3
18:00 Cardiff v West Brom
Chelsea 1 v Crystal Palace 1*
18:00 Everton v Fulham
18:00 Newcastle v Southampton
18:00 West Ham v Sunderland
20:30 Hull V Stoke
Jumapili Desemba 15
16:30 Aston Villa v Man United
16:30 Norwich v Swansea
19:00 Tottenham v Liverpool

No comments:

Post a Comment