Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, May 4, 2013

AZAM YATOLEWA KWENYE MASHINDANO YA KOMBE LA SHIRIKISHO BARANI AFRIKA BAADA YA KUFUNGWA 2-1 NA AS FAR RABAT



TIMU ya Azam FC leo imefungwa mabao 2-1 AS FAR Rabat kwenye mchezo wa kombe la Shirikisho barani mchezo uliochezwa Uwanja wa Prince Moulay Abdellah nchini Morocco

Azam ilihitaji sare yoyote ya mabao ili iweze kufuzu lakini dakika ya 81 ilipata penalti ikiwa nyuma kwa mabao 2-1, lakini fundi wa upigaji wa michomo hiyo, John Raphael Bocco alikwenda kugongesha mwamba mpira huo na kurudi uwanjani.

Azam ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao dakika ya sita, mfungaji John Raphael Bocco kwa mpira wa adhabu, baada ya beki mmoja wa AS FAR Rabat kushika mpira kwenye eneo la hatari.

Iliwachukua dakika sita tu AS FAR Rabat kusawazisha kupitia kwa Abdelrahim Achchakir kwa mkwaju wa penalti, baada ya beki David Mwantika kumchezea rafu mchezaji wa AS FAR Rabat.

Abdelrahim Achchakir alitolewa nje kwa kuonyeshwa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu Brian Umony dakika ya 35 lakini SA FAR Rabat wakiwa pungufu waliongeza bao la pili kupitia kwa Mustafa Allaoui alipiga vizuri shuti la mpira wa adhabu dakika ya 42.

Kipindi cha pili, mchezo ulizidi kuwa wa kasi na  kushambuliana kwa zamu na dakika ya 56 beki wa Azam David Mwantika kutolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu mchezaji wa AS FAR Rabat. Na Waziri Salum alionyeshwa kadi nyekundu dakika ya 75 baada ya kumchezea rafu Kaddioiu Yuossef.

Pamoja na Azam kuwa pungufu waliendelea kulishambulia lango la AS FAR Rabat na dakika ya 81 beki wa AS FAR Rabat alishika mpira kwenye eneo la hatari na mwamuzi akamuru penalti ambayo Bocco alikosa baada ya shuti lake kugonga mwamba.

Azam imetolewa kwa jumla ya mabao 2-1, baada ya mchezo wa awali wiki mbili zilizopita kutoka sare ya bila kufungana Dar es Salaam na Waarabu hao.

Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Mwadini Ally, Himid Mao, Waziri Salum, David Mwantika, Joackins Atudo, Kipre Balou, Kipre Tchetche, Salum Abubakar, John Bocco, Humprey Mieno/Gaudence Mwaikimba dk79  na Brian Umony/Khamis Mcha dk70.

AS FAR Rabat; Ali Grouni, Anouar Younes/Ennajar Tarik, Younes Hammal, Younes Belakhdar, Kaddoui Youssef, Abdelrahim Achchakir, Aqqal Salaheddine/Alloudi Soufiane, Mustafa Allaoui, El Kodry Yassine, El Bakkali Medamine na El Yousfi Mostafa.

No comments:

Post a Comment